Kazi kubwa ya Kitengo cha Mipango ni kusimamia na kuratibu mipango na Bajeti ya Ofisi ya Msajili wa Hazina. Aidha, kulingana na muundo wa Ofisi, kitengo kina majukumu yafuatayo:
Kuratibu matayarisho ya Bajeti, Mpango wa mwaka pamoja na kufuatilia utekelezaji;
Kusimamia ufuatiliaji na tathmini wa Shughuli za Msajili wa Hazina;
Kuandaa michango ya Ofisi katika Hotuba ya Bajeti pamoja na taarifa ya mwaka ya Uchumi;
Kuwajengea uwezo watumishi katika maeneo ya Mpango Mkakati, bajeti na mfumo wa ufuatiliaji na tathmini;
Kuratibu mapitio ya Sera za Ofisi ya Msajili wa Hazina na kuzihuisha ili ziendane na Sera za kitaifa;
Kupitia na kutoa ushauri juu nyaraka mbalimbali za kisera kutoka kwenye Taasisi na Mashirika ya Umma;
Kutayarisha makubaliano ya Awali (MOU) kwenye miradi/Programu ili kupata fedha za nje;
Kuratibu shughuli za Bunge zinazohusu utendaji wa Mashirika na Taasisi za Umma;
Kutayarisha miradi ya Ofisi ya Msajili wa Hazina, Mpango kazi na kufuatilia utekelezaji wake;
Kuibua mikakati ya kutafuta rasilimali fedha za kuendesha Ofisi;
Kufanya utafiti wa awali kuhusu utoaji wa huduma ili kupata maoni ya wadau juu ya huduma zitolewazo na kuishauri menejimenti; na
Kuratibu mapitio ya utendaji wa nusu mwaka na wa mwaka wa Ofisi ya Msajili wa Hazina .