FEDHA NA UHASIBU
MAJUKUMU
- Kuandaa ripoti za Mapato na Matumizi za mwezi, robo mwaka na za mwaka mzima
- Kufanya malipo mbalimbali ya kimkataba na ya kawaida.
- Kumshauri Afisa Masuhuli kuhusu masuala ya Kifedha.
- Kupokea maduhuli na kukatia risiti.
- Kupokea hati ya mgao wa fedha (Exchequer) na kukatia risiti.
- Kufanya Usuluhisho wa benki (bank reconciliation).
- Kuandaa Mishahara ya watumishi wa ofisi na kuwasilisha makato mbalimbali ya Taasisi husika (Statutory and Non Statutory Deductions).