• Jumatatu – Ijumaa Saa 1:30Asb – 9:30Alasiri

  • WALIOTEMBELEA

  • Utawala na Rasilimali Watu

    MAJUKUMU YA UTAWALA NA RASILIMALI WATU

    1. Kusimamia Rasilimali Watu na majukumu ya kiutawala katika Ofisi ya Msajili wa Hazina,
    2. Kuratibu taratibu za ajira, malipo, tathmini ya utendaji, promotions, ustawi wa wafanyakazi, motisha, mahitaji ya mafunzo, terminations, stahiki na kuhakikisha kwamba Kanuni za Utumishi zinafahamika na kufuatwa,
    3. Kutafsiri Kanuni za Utumishi wa Umma, Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma, Sheria za Kazi na kanuni zake, na kuhakikisha kwamba zinazingatiwa na kutekelezwa,
    4. Kuhakikisha kwamba kuna mahusiano mazuri katika eneo la kazi na kwamba migogoro yote inatatuliwa mara moja na ipasavyo,
    5. Kuhakikisha kwamba Msajili wa Hazina ana mfumo bora wa utoaji tuzo kwa watumishi, sera za malipo na kuhakikisha kwamba kuna taratibu bora za kuwahamasisha watumishi,
    6. Kutoa ushauri juu ya maendeleo ya watumishi, usimamizi wa utendaji na usimamizi wa kazi kwa watumishi wa Msajili wa Hazina;