Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

OFISI YA MSAJILI WA HAZINA

Ofisi ya Msajili wa Hazina yakabidhi rasmi mashamba
04 Jul, 2022
Ofisi ya Msajili wa Hazina yakabidhi rasmi mashamba

NAIBU Waziri Wizara ya Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe (Mb) ameitembelea Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) na kuipongeza menejimenti pamoja na watumishi wake na kusikiliza kazi na majukumu ya taasisi pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo.

Katika taarifa yake Mhe. Naibu Waziri ameeleza jinsi taasisi hii ilivyoleta mageuzi ya kiuchumi mara baada ya kuanzishwa kwa Mfumo wa Stakabadhi (Warehouse Receipts System) ambao umesaidia wakulima kuondokana na changamoto mbalimbali ikiwemo changamoto ya bei, ubora wa mazao, wizi n.k

Mhe. Kigahe ameeleza kuwa licha ya uchache wa watumishi katika taasisi hii, watumishi wanapaswa kuendelea kufanya kazi kwa juhudi na kushirikiana na Taasisi nyingine zinazofanya kazi zinzoendana kwani Bodi ndio inayotegemewa na wakulima na wazalishaji wa bidhaa hasa kupitia utaratibu wa stakabadhi ghalani, mfumo ambao umeleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi katika nchi yetu.

“Ushirikiano ni muhimu kati ya Bodi, Tume ya Maendeleo ya Ushirika na Soko la Bidhaa na wadau wengine ambapo hii itasaidia kufanikiwa kwa mfumo na kutatua changamoto zinazojitokeza kwa sasa” Amesema Mhe. Kigahe.